Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Vichokochoko vimeanza, msiingizwe mkenge
Habari za Siasa

Rais Samia: Vichokochoko vimeanza, msiingizwe mkenge

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania, amewataka wananchi kudumisha amani na kuwaepuka walioanzisha “vichokochoko” kuwapuuza kwani hawawatakii mema. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Rais Samia ametoa onyo hilo, jana Jumatano, tarehe 7 Julai 2021, alipokuwa akizungumza na wananchi wa Msamvu, mkoa wa Morogoro akisema, amani iliyopo nchini diyo msingi mkuu wa maendeleo ya taifa lolote duniani.

“Niwaombe sana ndugu zangu, vijichokochoko, vimeanza lakini naomba msivipokee, wanaokuja na vichokochoko wameshajua matumbo yao yanajaaje, chakula chao wanatoa wapi, pesa za matibabu watatoa wapi.”

“Nawaomba sana, wasije wakawaingiza mkenge. Kwa sababu pakichafuka ni wewe ndiyo utakaa ndani na mama watoto, msijue mtoto akiumwa utakwenda kumtibu na pesa gani,” alisema Rais Samia

Amri Jeshi Mkuu huyo alisema, “niwaombe sana tuendelee kuilinda amani na zinapotokea fujo, tunazijabili kwa haraka ili mambo yaendelee vizuri. Tuizunde amani yetu.”

Aidha, Rais Samia aliwataka wananchi wa eneo hilo na Watanzania kwa ujumla kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona kwa kufuata maelekezo ya wataalam wa afya ili kuepuka kupata maambuzi ya ugonjwa huo.

Rais Samia alisema baadhi ya maeneo nchini kama Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Dodoma tayari yana wagonjwa wa corona hivyo ni vyema wananchi wakafuata maelekezo ya wataalam.

Pia, aliwapongeza wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuwa sehemu ya miradi mikubwa miwili ya kimkakati ya Reli ya Kisasa (SGR) na Mradi wa Kufua Umeme wa Mwalimu Nyerere katika mto Rufiji.

Alisema kutokana na kuwepo kwa miradi hiyo mkoani Morogoro ni vyema wananchi wakawa walinzi ili iweze kuwanufaisha wao na taifa kwa ujumla.

Aidha, Rais Samia amewahakikishia wakazi wa mkoa wa Morogoro kuwa changamoto mbalimbali zinazowakabili zikiwemo uhaba wa maji, migogoro ya ardhi, masuala ya afya na mengineyo kuwa serikali tayari imeshazifanyia kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

error: Content is protected !!