Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia: Trilioni 1.3 zibaki, kilio wakandarasa sasa basi
Habari

Rais Samia: Trilioni 1.3 zibaki, kilio wakandarasa sasa basi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameagiza watekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi wa shule na maji nchini, kuwatumia wakandarasi wa ndani kwa kuwa miaka mingi wamekuwa wakilia kutopata zabuni kutoka serikalini. Anaripoti Mwandishi wetu (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Oktoba, 2021 jijini Dodoma wakati akizindua kampeni ya maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika hilo la IMF.

Amesema hatua hiyo itasaidia kuhakikisha fedha hizo zinabaki nchini.

“Zinapaswa kuzunguka ndani ya uchumi wa nchi hapa na zisitoke nje.

“Wakandarasi sasa kazi hizi hapa, tunaomba sana wenyewe wakawe wakandarasi wenye sifa, wakandarasi bora ambao watafanya kazi kwa umakini, ufanisi na uwajibikaji mkubwa. Nawatetea ili fedha hii ilipwe kwao iweze kuzunguke kwenye uchumi wa hapa nchini,” amesema.

Pia ametoa rai kwa wasimamizi wa miradi hiyo kwamba wazingatie muda wa utekelezaji wa program hiyo ambayo ni miezi tisa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!