Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia: Tozo za Sept, Oktoba kujenga madarasa 500
HabariTangulizi

Rais Samia: Tozo za Sept, Oktoba kujenga madarasa 500

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, tozo zitakazotozwa katika miamala ya simu Septemba na Oktoba 2021, zitakwenda kujenga vyumba vya madarasa zaidi ya 500 nchi nzima. Anaripoti Vicktoria Mwakisimba, TUDARCo…(endelea).

Tozo hizo zilianza kutozwa tarehe 15 Julai 2021 ambapo hadi kufikia 30 Agosti 2021, zaidi ya Sh.60 bilioni zilikuwa zimekusanywa na kupelekwa kujenga miradi ya sekta ya afya.

Akizungumza na wananchi wa Tegeta, mkoani Dar es Salaam akiwa njiani kwenda Bagamoyo Mkoa wa Pwani, leo asubuhi Alhamisi, tarehe 2 Septemba 2021, Rais Samia amesema, lengo ya tozo hizo ni kutekeleza miradi ya maendeleo.

“Miradi ya maendeleo, tutaimaliza kama tulivyopanga na nataka kuwahakikishi, tutakwenda kuitekeleza kama tulivyopanga na huko nyuma tulikuwa tunaitekeleza tukipata misaada, lakini sasa tunaitekeleza kwa fedha zetu,” amesema Rais Samia

“Tuliweka tozo kwenye mambo ya fedha za mitandao, yamepigiwa kelele sana, nimesikia na tumekaa na wataalamu na kupunguza asilimia 30, nataka kuwaeleza tozo zitaendelea kuwepo na wala sitawaficha,” amesema .

Amesema, toka tumeanza kutekeleza tumekusanya zaidi ya bilioni 60 na tunatekeleza miradi yetu sisi wenyewe na kama mnavyojua, Januari tuna wimbi kubwa la watoto wanaotaka kuingia darasa la kwanza.

“Fedha tutakazozikusanya mwezi huu wa Septemba na Oktoba, tunakwenda kujenga madarasa zaidi ya 500 nchi nzima,” amesema

Kuhusu ombi la Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima la kujengwa kwa shule, Rais Samia amesema “Shule iliyoombwa hapa itakwenda kujenga na kitakachokusanywa miezi miwili ijayo, itakwenda kujenga.”

“Sasa wanadamu ukifanya watasema na usipofanya watasema, bora tufanye waseme wakione kuliko kutokufanya wakasema,” amesema huku akisisitiza

“misaada siku hizi ni michache sana, lazima tuminyane sisi wenyewe.”

Kuhusu safari yake hiyo ya Bagamoyo amesema “unakwenda katika vivutio mbalimbali, tunakwenda kuitangaza Tanzania ulimwenguni na tutakwenda kuizindua filamu yetu Marekani na itafungua milango ya kuitangaza zaidi Tanzania na itatuonyesha tunavyoishi, tulivyo, siasa zetu na wanaopeleka uongo utafahamika.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!