Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia, Spika Ndugai wateta Ikulu
Habari za Siasa

Rais Samia, Spika Ndugai wateta Ikulu

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la nchi hiyo, Job Ndugai. Anaripoti Matilda Peter, Dodoma … (endelea).

Mazungumzo hayo, yamefanyika leo Jumanne, tarehe 20 Aprili 2020, Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma.

Rais Samia, amefanya mazungumzo na kiongozi huyo wa Bunge, ikiwa ni siku moja imesalia, kabla ya kulihutubia Bunge.

Keshokutwa Alhamisi, Rais Samia atakihutubia Bunge la Tanzania, kwa mara ya kwanza, tangu alipoingia madarakani tarehe 19 Machi 2021.

Iliingia madarakani baada ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli, kufariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa nyumbani wake, Chato mkoani Geita.

Bunge hilo la 12, lilizinduliwa na Hayati Magufuli tarehe 13 Novemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!