Wednesday , 17 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia: Polisi tumieni Tehama kudhibiti uhalifu
Habari Mchanganyiko

Rais Samia: Polisi tumieni Tehama kudhibiti uhalifu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amelitaka jeshi la polisi kujipanga vizuri kwenye masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano (Tehama) ili kudhibiti matukio ya uhalifu kikamilifu. Anaripoti Mwanaharusi Abdallah TUDARCo … (endelea).

Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Jumatano tarehe 25 Agosti 2021 wakati akifungua kikao kazi cha maofisa wakuu waandamizi wa jeshi la polisi na makamanda wa polisi wa mikoa/vikosi – Oysterbay Dar es salaam.

Amesema katika siku za karibuni masuala ya uhalifu yamekuwa yakihusisha teknolojia hususani matukio ya wizi kwa njia ya mtandao.

Pia, amesema Tehama hutumiwa zaidi na wahalifu wa ugaidi hivyo ni vema jeshi la polisi nalo likabadilika na kujiimarisha katika matumizi ya Tehama ili kubaini wahalifu hao kwa urahisi.

Aidha, ameliagiza jeshi hilo kukemea na kuwakamata wafanyabiashara wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Sekta binafsi yasifu utekelezaji wa Mkumbi

Spread the loveSERIKAL imepongezwa kwa utekelezaji wa mapendekezo ya sekta binafsi kupitia...

Habari Mchanganyiko

Kamati ya bunge yapigia chapuo kilimo ikolojia

Spread the loveSERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo imeshauriwa kushirikiana na wadau wa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili

Spread the loveSERIKALI imepata hasara ya kiasi cha Sh. 111.76 milioni, baada...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!