Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia: Niombeeni nikidhi matamanio ya Watanzania
Habari Mchanganyiko

Rais Samia: Niombeeni nikidhi matamanio ya Watanzania

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amewaomba viongozi wa dini waendelee kuiombea Serikali ili aendelee kuongoza kwa uadilifu, haki pamoja na kukidhi matamanio ya Watanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi, ametoa wito huo leo Jumanne, akizungumza na viongozi wa dini walioshiriki kongamano la kumuombea lililofanyika jijini Mbeya, kwa njia ya simu.

“Kwa hiyo mimi niwashukuru viongozi wa dini na kamati zote za amani, niwatie moyo muendelee kunifanyia hivyo. Mliombee Taifa, mtuombee na viongozi tuweze kuongoza kwa uadilifu, tuongoze kwa haki, tuongoze kama matamanio ya Watanzania. Nategemea ushirikiano wenu,” amesema Rais Samia na kuongeza:

“Nawashukuru sana kwa kongamano mnalofanya, nashukuru sana kwa kweli Taifa linawategemea sana viongozi wa dini kwa maombi, sala na dua zenu. Ndiyo maana tunaweza kufanya tunayofanya.”

Akijibu salamu hizo, Mwenyekiti wa Kongamano la Viongozi wa Dini la Kumuombea Rais Samia, Askofu Donald Mwanjoka, amesema wamechukua hatua hiyo baada ya kuguswa na uongozi wake.

“Nasi tunafanya hivyo tumeguswa na uongozi wako unavyoongoza tangu umeingia madarakani. Tumekusanyika hapa tuendelee kuubeba mpaka tunafika mahali tunasema kwamba ingekuwa kuna rais wa dunia, tungekuchagua uwe rais wa dunia,” amesema Askofu Mwanjoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!