Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Tangulizi Rais Samia: Ni vibaya kutumia dini kufanya siasa
Tangulizi

Rais Samia: Ni vibaya kutumia dini kufanya siasa

Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania, amewaomba viongozi wa dini nchini humo, kutokutumia nafasi zao kufanya siasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).

Rais Samia ametoa nasaha hizo, leo Alhamisi, tarehe 8 Julai 2021, wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), unaofanyika Kilakala, Mkoa wa Morogoro.

Amesema, viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika jamii kwani wanayoyasema yabaki mioyoni mwa waumini wao tofauti na yale yanayosemwa na wanasiasa.

“Wakati mwingine dini na siasa ni vitu vinakwenda sambamba na wakati mwingine vinakinzana, inategemea mtu anaitumiaje, lakini kuna ubaya unapoitumia dini ile kufanya siasa,” amesema Rais Samia

Aidha, ametumia fursa hiyo, kuwaomba viongozi wa dini, kuhakikisha wanatumia nafasi yao kuwasisitiza waumini kuendelea kuchukua tahadhari ya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

“Nawaomba maaskofu na viongozi wengine wa dini, kuendelea kuwakumbusha waumini wenu kuendelea kuwasisitiza umuhimu wa kujikinga na corona,” amesema Rais Samia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

Habari za SiasaTangulizi

Mawakili wa Chadema wabadilishia gia angani

Spread the loveMAWAKILI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameiomba Mahakama...

Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Jesca Kishoa avunja ndoa na Kafulila

Spread the love  NDOA baina ya Jesca David Kishoa, mbunge wa Viti...

error: Content is protected !!