Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Rais Samia: Ni vibaya kutumia dini kufanya siasa
Tangulizi

Rais Samia: Ni vibaya kutumia dini kufanya siasa

Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania, amewaomba viongozi wa dini nchini humo, kutokutumia nafasi zao kufanya siasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).

Rais Samia ametoa nasaha hizo, leo Alhamisi, tarehe 8 Julai 2021, wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa 31 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), unaofanyika Kilakala, Mkoa wa Morogoro.

Amesema, viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika jamii kwani wanayoyasema yabaki mioyoni mwa waumini wao tofauti na yale yanayosemwa na wanasiasa.

“Wakati mwingine dini na siasa ni vitu vinakwenda sambamba na wakati mwingine vinakinzana, inategemea mtu anaitumiaje, lakini kuna ubaya unapoitumia dini ile kufanya siasa,” amesema Rais Samia

Aidha, ametumia fursa hiyo, kuwaomba viongozi wa dini, kuhakikisha wanatumia nafasi yao kuwasisitiza waumini kuendelea kuchukua tahadhari ya maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

“Nawaomba maaskofu na viongozi wengine wa dini, kuendelea kuwakumbusha waumini wenu kuendelea kuwasisitiza umuhimu wa kujikinga na corona,” amesema Rais Samia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!