Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Mwanamke sio mtu wa daraja la pili
Habari za Siasa

Rais Samia: Mwanamke sio mtu wa daraja la pili

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameliomba Kanisa la Anglikana Tanzania kuunga mkono dhamira ya Serikali katika kuwainua wanawake kijamii, kiuchumi, kisiasa na kupambana na ukatili, dharau, kejeli na manyanyaso wanayokabiliana nayo. Anaripoti Helena Mkonyi – TUDARCo.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 28 Septemba 2021 jijini Dodoma wakati akihutubia katika maadhimisho ya miaka 50 ya Kanisa la Anglikana Tanzania.

Amesema si kwamba serikali imedhamiria kutetea wanawake kwa sababu yeye ni mwanamke bali kwa sababu mwanamke ni kiumbe mwenye haki sawa na mwingine anayezaliwa na binadamu.

“Tunapozaliwa wote tunatoka sawa, kwani kuna mwanaume anasema ametoka na shape ya kichwa yenye akili zaidi, wote tunazaliwa sawa. Kinachotutofautisha ni makuzi na imani katika makabila yetu. Katika mambo mengine, mwanamke ana haki sawa na mwanaume kwenye jamii.

“Tunakubali kuna haki za ki-Mungu, mimi nabeba mimba najifungua… wewe huwezi, kwa hilo nina fahari kwamba Mungu amenipa heshima ya kuleta viumbe duniani, unachofanya wewe ni kunichangia mbegu yako, lakini mengine yote ninafanya mwenyewe, kwa makabila mengine mtoto ni wa mama sio wa baba.

“Kwa hiyo mzigo huo alionipa Mungu ni mkubwa na ni heshima kubwa lazima niheshimiwe kwa sababu nimewaleta mimi, nimewakuza mimi, ukiumwa ni mimi, shibe na raha yako ni mimi.

“Sasa unaponiona kama ni mtu wa daraja la pili, sikuelewi nami nitasimama na hilo, kuwanyanyua wenzangu tuende pamoja, lakini sisi wanawake ni zaidi ya asilimia 50 kwenye nchi hii, mkituacha nyuma, nchi itaendelea lini? Alihoji Rais Samia.

Alisema katika malengo ya kimataifa hakuna mtu ambaye anatakiwa aachwe nyuma kimaendeleo.

“Sasa mnapodogosha wanawake mkawanyima haki zao, mkawaonea kwenye mirathi, mkawanyang’anya ardhi zao maendeleo yanakuja lini?

“Nguvu za kanisa isiwe tu kwenye kuwakopesha wanawake na kulea ma-yatima, lakini pia kujenga heshima ya mwanamke wa Tanzania. Kanisa liseme kwa sauti kubwa. Baba Askofu nomba mniunge nguvu kwenye hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha, Askofu Mkuu wa Anglikana Tanzania, Maimbo Mndolwa amesema kanisa hilo linaendelea kuwainga mkono wanawake kwa kuwawezesha kupata mikopo mbalimbali ili kujikwamua kiuchumi

1 Comment

  • Mama, umetema cheche za kweli. Mwafrika wa kwanza kupata PH. D. ni Dk. James Aggrey wa Ghana. Yeye aliwahi kusema, “Ukimwelimisha mwanaume, unamwelimisha mtu mmoja, lakini ukimwelimisha mwanamke, unaielimisha familia nzima.”
    Wakati unakwazwa, kumbuka haya, useendelee kutumia watu waliopita. Tafuta watu wapya kabisa wanaokuunga mkono.
    Kila unapochagua watu wa enzi za nyuma, wananchi wanamwona kiongozi aliyetangulia, siyo wewe. Endelea na watu wa JPM halafu waweke watu wako wapya. Ubarikiwe kwa mema utakayoyafanya kwa Tanzania.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!