Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia mgeni rasmi Siku ya Maridhiano
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia mgeni rasmi Siku ya Maridhiano

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Maridhiano day yatakayofanyika tarehe 3 Machi mwaka huu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jana tarehe 28 Februari, 2022 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania, Sheikh Alhaji Mussa Salumu ambaye pia ni Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema jumuiya hiyo inatimiza miaka 6.

Amesema Jumuiya hiyo ilisajiliwa rasmi tarehe 3 Machi, 2016 lengo likiwa ni kushirikiana na serikali kuhimiza amani na utulivu kwa watanzania wote.

Amesema Jumuiya ya maridhiano Tanzania ni jumuiya inayoudwa na viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali hapa nchini Tanzania bila kujali itikadi ya chama wala dini yoyote.

“Malengo ya Jumuiya ya maridhiano ni kuleta mwafaka katika mambo yanayosababisha tofauti katika dini, mila, siasa na madhehebu mbalimbali ya dini.

“Kusaidia juhudi za serikali katika jitihada zake za kuondoa au kupunguza umasikini, kama ile ya wakulima na wafugaji,” amesema Mwenyekiti.

Aidha, amesema katika maadhimisho ya wiki ya maridhiano day wamekuwa wakichangia damu takribani nchi nzima kwa lengo la kuwasaidia watu wenye uhitaji.

“Hii ni siku ya ambayo wana maridhiano wa nchi nzima tumekubaliana kuiadhimisha kwa uchangiaji wa damu ili kuokoa maisha ili kuokoa maisha ya mama na mtoto, watu waliopata ajali na wagonjwa mbalimbali.

“Hili ni zoezi ambalo litahitimishwa siku ya tarehe 03 Machi 2022 kwa shughuli maalum katika ukumbi wa itakayofanyika katika ukumbi wa Jakaya Kikwete Concentration Centre hapa mjini Dodoma, kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa saba 7 mchana” amesema Mwenyekiti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!