RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassa amekutana na kuzungumza na Makamu Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani nchini humo- Chadema, Tundu Lissu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Wawilli hao wamekutana leo Jumatano, tarehe 16 Februari 2022 nchini Ubelgiji. Rais Samia yupo huko ziarani huku Lissu akiishi huko tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu 2020.
Taarifa ya Zuhura Yunus, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, Rais Samia amekutana na mwanasiasa huyo ambaye aliomba kumwona kiongozi wake mkuu wa nchi.
Zuhura amesema, Rais Samia na Lissu wamezungumza masuala mbalimbali yenye maslahi mapana ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Leave a comment