Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Rais Samia kwenda ziarani Kenya
Habari Mchanganyiko

Rais Samia kwenda ziarani Kenya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Saluhu akihutubia Taifa mara baada ya kuapishwa
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kwenda nchini Kenya kwa ajili ya ziara ya siku mbili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa Kanze Mararo, Msemaji wa Ikulu nchini Kenya, ziara hiyo inatarajiwa kuanza tarehe 4 Mei 2021 ambapo Rais Samia atafanya mazungumzo na Rais Uhuru Kenyatta wa taifa hilo

Alipoulizwa na chombo kimoja cha habari nchini kuhusu safari hiyo, Gerson Msigwa ambaye ni Msemaji wa Ikuli ya Tanzania, amesema Wizara ya Mambo ya Nje ndio wenye jukumu hilo.

Emmanuel Buhohela, Ofisa Habari wa Wizara ya Mambo ya Nje, amesema waziri atalizungumzia hilo.

Gerson Msigwa mkuu wa idara ya habari na maelezo

Tarehe 22 Machi 2021, akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya taifa lake jijini Dodoma, wakati wa kuaga mwili wa Hayati John Magufuli, Rais Kenyatta alimkaribisha Rais Samia nchini kwake.

Hata hivyo, tarehe 10 Aprili 2021, Kenyatta alituma ujumbe maalumu nchini ulioongozwa na Waziri wa Michezo, Utamaduni na Urithi wa nchi hiyo, Balozi Amina Mohamed.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!