Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kuunda kamati ya ushauri marekebisho ya Katiba
Habari za Siasa

Rais Samia kuunda kamati ya ushauri marekebisho ya Katiba

Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake imedhamiria kuukwamua mchakato wa marekebisho ya katiba na kwamba muda si mrefu kamati ya ushauri juu ya namna ya kuuendesha itaundwa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi ametoa ahadi hiyo leo Jumanne, tarehe 3 Januari 2023, akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa nchini Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.

“Nataka kuwaambia Serikali inadhamiria kukwamua mchakato wa marekebisho ya katiba kwa jinsi tutakavyokuja kukubaliana hapo mbele, lakini tuko tayari kuukwamua ili tuanze sasa kamati kadhaa zifanye kazi kuangalia mambo kadhaa,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema mchakato huo utakwenda kulingana na hali halisi ya sasa, kwa kuja na mambo mapya pamoja na kuchukua mazuri yaliyokuwepo kwenye Rasimu ya Katiba ya Jaji Joseph Warioba na katiba pendekezwa.

“Wengine wanasema tuanze na katiba ya Jaji Warioba, wengine katiba pendekezwa lakini ile ilikuwa 2014 ni miaka nane imepita mambo kadhaa yamebadilika. Lakini kuna mambo yamebadilika wakati ule yalikuwa yanatuongoza, kuna haja ya kuangalia hali halisi ya sasa ikoje,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema kamati ya ushauri juu ya namna ya kufufua marekebisho ya katiba mpya, itakuwa na wajumbe kutoka kwenye makundi mbalimbali, ikiwemo vyama vya siasa, mashirika yasiyo ya kiserikali, na watanzania wanaofanya kazi katika taasisi za kimataifa.

Aidha, amesema mchakato wa marekebisho ya katiba utafanyika kwa ustaarabu ili kuruhusu shughuli nyingine za maendeleo kuendelea.

“Nataka niwaambie hakutakuwa na kamati itakayokuwa, vuguvu leo wapi twendeni wapi leo.Tutakuwa na kamati itakayofanya kazi zake kwa maelekezo tutakayowapa kwamba hadidu rejea ni hizi 12 nendeni yafanyieni kazi. Pahali wapi tutawapangia vizuri tu, lakini sio lile vuguvugu,” amesema Rais Samia na kuongeza:

“Tunataka wakati mchakato unaendelea nchi iko tulivu inaendesha shughuli zake za maendeleo na sio vuguvu ambalo litakwenda kusimamisha kila kitu tunaangalia wote kwenye katiba. Watanzania hawatakuja kushiba kwenye katiba, ikiingia njaa wakulima watakuja kunipigia kelele.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!