Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kung’oa vikwazo vya uwekezaji
Habari za Siasa

Rais Samia kung’oa vikwazo vya uwekezaji

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameahidi kufanya marekebisho kadhaa katika sera na sheria sambamba na kuondoa vikwazo katika kukuza uwekezaji. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Akihutubia Bunge kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kushika mamlaka ya juu ya nchi leo tarehe 22 Aprili 2021, Rais Samia amesema, serikali yake itaendelea kuboresha sera za fedha ili kudhibiti sarafu ya Tanzania.

“Tutafanya marekebisho kadhaa katika sera, sheria na kuondoa vifungu vitakavyokuwa vikwazo katika kukuza uwekezaji.

“Tutaendelea kuboresha sera za fedha kuhakikisha viashiria vyote vya uchumi kama mfumuko wa bei unadhibitiwa, sambamba na kukuza thamani ya sarafu,” amesema.

Amesema, kwa sasa kumekuwa na mzunguko mkubwa kwa wawekezaji pale wanapotaka kuwekeza, na kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inataka uwekezaji wa haraka.

“Ndani ya nchi yetu, kumekuwa na mizunguko mikubwa watu wanapokuja kwa ajili ya uwekezaji, Serikali ya Awamu ya Sita tunakwenda kukomesha hilo na uwekezaji utakwenda kufanyika kwa haraka,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!