RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ameweka shada la maua kaburi la aliyekuwa Rais wa Taifa hilo, Hayati John Pombe Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea).
Ni leo Alhamisi, tarehe 14 Oktoba 2021, nyumbani kwa Hayati Magufuli, Chato mkoani Geita.
Rais Samia amefika nyumbani kwa Hayati Magufuli akiwa njiani kwenda Uwanja wa Magufuli, kuhudhuria kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru 2021.
Magufuli, alifikwa na mauti saa 12 jioni ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, iliyopo Makumbusho jijini Dar es Salaam na mwili wake, kuzikwa 26 Machi 2021.
Mara baada ya kifo hicho, Samia aliyekuwa Makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais tarehe 19 Machi 2021.
Leave a comment