Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia awataka wananchi wapige kelele changamoto za afya
Habari za Siasa

Rais Samia awataka wananchi wapige kelele changamoto za afya

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka wananchi kupaza sauti zao wanapokutana na changamoto za huduma ya afya, ili Serikali yake izifanyie kazi. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Kiongozi huyo wa Tanzania, ametoa wito huo leo Jumanne tarehe 1 Juni 2021, alipofanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala, mkoani Dar es Salaam.

Rais Samia alitoa kauli hiyo baada ya kugawa mashuka 200, katika hospitali hiyo.

“Hospitali iko vizuri na mimi nimetoa zawadi kidogo ya mashuka 200, ili wagonjwa wetu walale vizuri. Sasa mkikuta mashuka yamechanika chanika, wagonjwa wamelazwa, pigeni kelele tusikie. Sababu mashuka 200 si haba,” amesema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia amesema Serikali yake inaendelea kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya afya nchini, ikiwemo upungufu wa dawa na vifaa tiba.

“ Lakini nitaenda kwenye hospitali nyingine kurekebisha mambo, nimesikia upungufu wa dawa jambo ambalo nakwenda kulifanyia kazi. Kuna mambo machache hayajakamilika, tunaenda kukamilisha,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!