Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo
Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Nape Nnauye, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Tekinolojia
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Tanzania kufanya kazi kitaaluma bila uoga, upendeleo na uonevu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro …(endelea).

Kauli imetolewa leo tarehe 29 Machi 2023 na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye kwa niaba ya Rais Samia wakati akifungua Mkutano wa 12 wa kitaaluma wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) unaofanyika mkoani Morogoro.

” Rais Dk. Samia anawasilimia sana, ameniambia, kazungumze nao waambie wafanye kazi kitaaluma bila woga, bila upendeleo wala uonevu, haya ni maneno yake mwenyewe,” amesema Waziri Nape.

Nape amesema Rais Dk. Samia ni muumini wa haki ya kujieleza na kutoa maoni, hivyo haoni sababu ya kuminya uhuru wa Habari.

“Rais alishawahi kuniambia wakati wa mchakato ya kupitia Sheria ya Habari kuwa tuhakikishe hatuingilii haki ya watu kujieleza.

“Nasi tumekuwa tukilifanya hilo, niwaombe kwa pamoja tutafsiri maono ya Rais wetu, yeye nia na dhamira yake ni kuona uhuru wa Habari unaleta tija kwa nchi,” amesema.

Pamoja mambo mengine, Waziri Nape amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa vyombo vya Habari ingawa anaamini wapo baadhi ya watu wanakwamisha, lakini watashughulika na watu wote wanakwamisha nia njema ya Rais ya kutaka kuwe na uhuru wa kweli wa Habari.

Katika mkutano huo Waziri Nape alikabidhiwa tuzo ya heshima na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) Deodatus Balile ikiwa ni tuzo ya kwanza ya heshima kupewa Waziri wa Habari tangu nchi hii kupata uhuru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!