RAIS Samia Suluhu Hassan amepongeza wasanii wawili wa sarakasi kutoka Tanzania, Ibrahim na Fadhili Ramdhan wanaounda kundi la The Ramadhan Brothers baada ya kuibuka washindi kwenye shindano la Australia’s Got Talent mwaka 2022 nchini Australia na kuzawadiwa USD 100,000 (Tsh. Milioni 230+). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Nawapongeza wanangu Ibrahim na Fadi (Ramadhan Brothers) kwa kipaji na ubunifu wenu wa kucheza sarakasi. Onesho lenu kupitia kipindi @GotTalentAU limeitangaza vyema nchi yetu ya Tanzania na nawatakia kheri katika kuendeleza sanaa yenu na kushiriki katika maonesho mbalimbali. pic.twitter.com/PivPFKgfvf
— Samia Suluhu (@SuluhuSamia) October 19, 2022
Kupitia akaunti yake ya Twitter leo tarehe 19 Oktoba, 2022, Rais Samia ameandika; “Nawapongeza wanangu Ibrahim na Fadi (Ramadhan Brothers) kwa kipaji na ubunifu wenu wa kucheza sarakasi. Onesho lenu kupitia kipindi @GotTalentAU limeitangaza vyema nchi yetu ya Tanzania na nawatakia kheri katika kuendeleza sanaa yenu na kushiriki katika maonesho mbalimbali.”
Leave a comment