RAIS Samia Suluhu Hassan amewatakia kheri wauguzi wote nchini katika kusherehekea siku ya wauguzi duniani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Katika ujumbe aliobandika kwenye ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 12 Mei, 2022 Rais Samia amesema Watanzania wanathamini mchango wa wauguzi katika kulinda afya ya wananchi.
“Tutaendelea kuwekeza zaidi katika sekta ya afya ili kuimarisha mazingira ya utendaji kazi pamoja na masilahi yenu.
Siku ya wauguzi husherehekewa tarehe 12 Mei kama siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa ya Florence Nightngale, mwana takwimu na mwanzilishi wa uuguzi wa kisasa.
Leave a comment