Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awapa milion 10 wafanyakazi Dawasa
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia awapa milion 10 wafanyakazi Dawasa

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa Sh.10 milioni kwa wafanyakazi bora wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (Dawasa) wa mwaka 2020/21. Anaripoti Ibrahim Yamola, Dar es Salaam … (endelea).

Ni mara baada ya Waziri wa Maji, Jumaa Aweso kumaliza kuwakabidhi tuzo wafanyakazi bora wa Dawasa, katika mkutano wa kufunga mwaka wa fedha 2020/21 kwa watumishi wa mamlaka hiyo. Dawasa inahudumia mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.

Alipoanza kuzungumza na wafanyakazi hao, Waziri Aweso amesema, “nawaletea salamu za Rais wetu mpendwa, anafuatilia mkutano huu. Anawapongeza sana.”

Huku ukumbi wa Diamond Jubilee, ulipofanyikia mkutano huo wakishangilia, Aweso akasema “Rais ametoa Sh.10 milioni kwa wafanyakazi bora wote.”

Mara baada ya kutangaza zawadi hizo, Waziri Aweso alimwita Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa, Mhandisi Cyprian Luhemeja naye kusogea kwenye kisemeo ‘MIC’ kutangaza zawadi zake.

Hata hivyo, Mhandisi Luhemeja, aliomba awasiliane kwanza na Mwenyekiti wa Bodi ya Dawasa, Jenerali mstaafu Davis Mwamunyange ambaye, baada ya kujadiliana kwa takribani nusu dakika, Mwamunyange alisogea kwenye kisemeo.

Huku wafanyakazi wa Dawasa zaidi ya 2,300 wakishangilia, Jenerali Mwamunganye alisema, “bodi imeamua kutoa Sh.200,000 kwa kila mfanyakazi.”

Miongoni mwa walitunukiwa ni tuzo ya kujitoa kwa mfanyakazi, Erasto Majuto ambaye alionekana Mei Mosi 2021, katika picha akiziba bomba lililopasuka wakati wa mvua.

Waziri Aweso alitumia picha hiyo katika ukurasa wake wa kijamii, kumpongeza Majuto akisema “nimemuona na kuguswa kipekee na mtumishi wa Dawasa, Erasto Majuto akipambana kudhibiti upotevu wa maji wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha jijini Dar Es Salaam.”

“Ni wazi anatimiza majukumu yake lakini ni moyo wa kizalendo kutokana na mazingira anayotekeleza hivyo kama motisha naahidi kumpa zawadi kama pongezi mtumishi huyu hasa leo ikiwa ni siku ya wafanyakazi.”

Leo Jumanne, kwenye mkutano huo, Waziri Aweso baada ya kumkabidhi tuzo amempongeza “kwani alifanya kazi ya kizalendo, wakati wa mvua na ninaomba CEO, nasikia Majuto hana mkataba, kama ana vigezo basi aajiliwe.”

Kisha alimwita mbele na kumpa tena zawadi ya fedha ambazo hazikujulikana haraka haraka ni kiasi gani.

Tuzo ya mfanyakazi bora wa Dawasa, imekwenda kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa mamlaka hiyo, Mhandisi Cyprian Luhemeja.

1 Comment

  • Kwa kuzingatia utawala bora, Afisa Mtendaji Mkuu ambaye pia ni CEO au Mwajiri hapaswi kuingia kwenye mambo ya mfanyakazi bora. Kwanza zawadi kama laki mbili haiwezi kuwa motisha kwake. Pili kazi zake zinasimamiwa na Bodi ya Wakurugenzi ambao wana mamlaka ya ama kumzawadia carrot au stick kulingana na matokeo ya utendaji wake katika kutoa huduma kwa wananchi. Tatu, anapaswa kusimamia vision ya taasisi na kuitekeleza kupitia Mpango Mkakati ulioidhinishwa na Bodi. CEO kuwa mfanyakazi bora kateuliwa na nani? Mwandishi hakujiongeza kutaka kujua aspect hiyo

    Halafu tabia hii ipo sana mamlaka za maji na nakumbuka mamlaka ya maji Arusha(AUWSA) CEO wake alijipa ufanyakazi bora mwaka 2011 jambo ambalo mwandishi wa Daily News wakati ule wa Arusha, Marc Valentine Nkwame alikiita kitendo hicho kuwa sawa na Daylight Robbery!
    Inaelekea ma CEO wengi hawajui mipaka yao na uzito wa nafasi walizopewa
    Mbaya zaidi, inaonyesha hata wajumbe wengi wa bodi hawajui mahitaji ya utawala bora maana hutaona wakichukua hatua yoyote kukemea hii tabia.
    Tubadilike sasa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!