Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia awamwagia pongezi Serengeti Girls
HabariMichezo

Rais Samia awamwagia pongezi Serengeti Girls

Rais Samia Suluhu Hassan akishuhudia mchezo kati ya Simba Na Yanga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameipongeza Timu ya Taifa hilo ya soka la Wanawake chini ya miaka 17 ‘Serengeti Girls’ kwa kufuzu kucheza Kombe la Dunia nchini India Oktoba 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Serengeti Girls walifuza jana Jumapili tarehe 6 Juni 2022 baada ya kuwaondoa Caremoon katika michezo miwili iliyopigwa.

Mchezo wa awali uliopigwa Cameroon, Sereengeti Girls iliibuka na ushindi wa 4-1 na ule uliipigwa jana Uwanja wa Aman Zanzibar ikaibuka na ushindi wa 1-0 hivyo kufuza kwa jumla ya magoli 5-1.

Hii ni mara ya kwanza Serengeti Girls inafuzu michuano hiyo mikubwa duniani.

Mara baada ya kufuzu, Rais wa Tanzania, Samia alitumia ukurasa wake wa Twitter kuwapongeza akisema, “nawapa Pongezi Timu ya Taifa ya Soka la Wanawake chini ya miaka 17 (Serengeti Girls) kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2022.”

“Hongera kwa benchi la ufundi na wote waliochangia kufikia hatua hii. Mmeweka historia kubwa na adhimu kwa nchi yetu. Ninyi ni fahari ya Watanzania.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!