Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Rais Samia awaapisha viongozi aliowateua
HabariTangulizi

Rais Samia awaapisha viongozi aliowateua

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua akiwemo Balozi Hussein Kattanga kuwa Katibu Mkuu Kiongozi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Viongozi hao wakiwemo mawaziri na naibu mawaziri, aliwateua jana Jumatano tarehe 31 Machi 2021.

Viongozi hao, wameapishwa leo Alhamisi tarehe 1 Aprili 2021, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali serikali na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini.

Mawaziri walioapishwa ni, Ummy Mwalimu kuwa Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi; Mohammed Mchengerwa (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) na Seleman Jafo (Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira).

Wengine ni, Prof. Palamagamba Kabudi (Katiba na Sheria), Dk. Mwigulu Nchemba (Fedha na Mipango), Dk. Kitila Mkumbo (Viwanda na Biashara), Goefrey Mwambe (Uwekezaji) na Balozi Liberata Mulamula (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki).

Naibu waziri walioapishwa ni, Naibu waziri Ofisi Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira, Hamad Hassan Chande, William Tate Olenasha (Uwekezaji), Abdallah Ulega (Mifugo na Uvuvi) na Mwita Waitara (Ujenzi na Uchukuzi).

Pia, Pauline Gekul (Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo), Mwanaidi Ally Hamid (Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto).

Wengine ni, Mhandisi Hamad Masauni (Fedha na Mipango), Balozi Mbarouk Nassoro Mbarouk (Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki).

Rais Samia amefanya mabadiliko hayo madogo ya baraza la mawaziri, siku kadhaa tangu alipochukua madaraka ya urais wa Tanzania, kufuatia kifo cha Hayati Dk. John Magufuli, aliyefariki dunia tarehe 17 Machi 2021.

Dk. Magufuli alifariki dunia kwa ugonjwa wa mfumo wa umeme wa moyo, katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, kisha mwili wake ulizikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

error: Content is protected !!