Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia awaapisha RC Shinyanga, Jaji kiongozi, Jaji Mahakama ya rufani
Habari za Siasa

Rais Samia awaapisha RC Shinyanga, Jaji kiongozi, Jaji Mahakama ya rufani

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaapisha viongozi watatu aliowateua tarehe 8 Oktoba 2021. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Viongozi hao wameapishwa leo Jumatatu, tarehe 11 Oktoba 2021 na Rais Samia, katika Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

Waliopaishwa ni Sofia Mjema, kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, akichukua nafasi ya Dk. Philemon Sengati, ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. Awali, Mjema alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha.

Kiongozi mwingine aliyeapishwa ni, aliyekuwa Jaji wa Mkuu wa Zanzibar, Jaji Omar Othman Makungu, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Tanzania.

Na, aliyekuwa Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma, Jaji Mustapha Siyani, kuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzaniua.

Jaji Siyani anachukua nafasi ya Jaji Eliezer Feleshi, aliyeteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali hivi karibuni (AG).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!