Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atua Z’bar, kushirki Karume Day
Habari za Siasa

Rais Samia atua Z’bar, kushirki Karume Day

Spread the love

 

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Jumanne, tarehe 6 Aprili 2021, amewasili Zanzibar akitokea jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Kesho Jumatano, Rais Samia atahudhuria maadhimisho ya Siku ya Mashujaa (Karume Day), itakayofanyika katika Ofisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kisiwandui.

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Abeid Amani Karume, Rais Samia amepokelewa na viongozi mbalimbali wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla.

Baadaye Rais Samia amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!