Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia atoa salamu za rambirambi kufuatia ajali ya ndege Bukoba
HabariKitaifaTangulizi

Rais Samia atoa salamu za rambirambi kufuatia ajali ya ndege Bukoba

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania Samia Suluhu ametoa pole kwa wafiwa na majeruhi wa ajali ya ndege iliyotokea Jumapili huko Bukoba, Kagera. Watu 19 walifariki katika ajali hiyo na wengine 26 kuokolewa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika ujumbe wake wa pole, Rais Samia pia amewashukuru wakazi wa Kagera kwa ujasiri, ushirikiano na jitihada walizofanya kuwaokoa abiria waliozama na ndege hiyo.

“Natoa pole kwa familia na wote walioguswa na vifo vya watu 19 waliopoteza maisha katika ajali ya ndege ya Precision iliyotokea Ziwa Victoria. Nawapongeza walioshiriki katika uokozi wakiwemo wananchi wa Bukoba. Nawaombea Marehemu wapumzike mahali pema na majeruhi wapone haraka.”

Ndege hiyo ilikuwa ikitoka Dar es Salaam kuelekea Bukoba kupitia Mwanza.

Precision Air ndiyo shirika kubwa la ndege la kibinafsi la Tanzania na kwa kiasi fulani inamilikiwa na Kenya Airways. Ilianzishwa mnamo 1993 na inaendesha safari za ndege za ndani na kikanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!