Wednesday , 17 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia atoa salamu za Eid
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia atoa salamu za Eid

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewatakia kheri ya Eid El Fitri Waislamu na Watanzania wote huku akiwataka kusherekea kwa amani na utulivu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia ametoa salamu hizo kupitia kurasa zake za kijamii leo Jumanne, tarehe 3 Aprili 2022.

“Kheri ya Eid kwenu nyote. Tusherehekee kwa amani na utulivu huku tukiiombea nchi yetu, tukikumbushana wajibu wa kushiriki katika ujenzi wa Taifa na kuendeleza mafunzo mema tuliyoyapata katika mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kutoka kwa Mtume wetu Muhammad (SAW). Eid Mubarak,” ameandika Rais Samia.

Aidha, mkuu huyo wa nchi, amewaongoza Watanzania katika kushiriki sala ya
Edd El Fitri, kitaifa iliyosaliwa Msikiti wa Mfalme, Muhammad wa Sita wa Morocco, ulioko Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Viongozi mbalimbali wa kisiasa na kiserikali wamehudhuria sala hiyo akiwemo Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari Mchanganyiko

Sekta binafsi yasifu utekelezaji wa Mkumbi

Spread the loveSERIKAL imepongezwa kwa utekelezaji wa mapendekezo ya sekta binafsi kupitia...

Habari Mchanganyiko

Kamati ya bunge yapigia chapuo kilimo ikolojia

Spread the loveSERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo imeshauriwa kushirikiana na wadau wa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yapata hasara 113 milioni hospitali kuwapa misamaha wagonjwa wasiostahili

Spread the loveSERIKALI imepata hasara ya kiasi cha Sh. 111.76 milioni, baada...

error: Content is protected !!