Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua wasaidizi wake 9
Habari za Siasa

Rais Samia ateua wasaidizi wake 9

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Saluhu akihutubia Taifa mara baada ya kuapishwa
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali kwenye ofisi yake akiwemo, Juma Selemani Mkomi kuwa katibu wake. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea). 

Uteuzi wa Mkomi umeanza tarehe 19 Machi, 2021.

Taarifa hiyo ya uteuzi, imetolewa jana usiku Ijumaa, tarehe 16 Aprili 2021, na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Pia, Msigwa amesema, Rais Samia amefanya uteuzi wa Wasaidizi katika Ofisi Binafsi ya Rais kama ifuatavyo;

1. Amemteua Said Ali Juma kuwa Mnikulu.

2. Amemteua Balozi Dk. Mussa Julius Lulandala kuwa Msaidizi wa Rais, Nyaraka na Ukalimani (PAP-TD).

3. Amemteua, Balozi Ali Bujiku Sakila kuwa Msaidizi wa Rais, Hotuba (PAP-SD).

4. Amemteua Maulidah Bwanaheri Hassan kuwa Msaidizi wa Rais, Diplomasia (PAP-DA).

5. Amemteua Felister Peter Mdemu kuwa Msaidizi wa Rais, Maendeleo ya Jamii.

6. Amemteua Nehemia Ernest Mandia kuwa Msaidizi wa Rais, Sheria (PAP-LA)

7. Amemteua Blandina Kilama kuwa Msaidizi wa Rais, Uchumi (PAP-EA).

8. Amemteua Dk. Salim Othman kuwa Msaidizi wa Rais, Siasa (PAP-PA).

Msigwa amesema, uteuzi wa Wasaidizi wa Rais umeanza jana Ijumaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!