Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua viongozi wawili
Habari za Siasa

Rais Samia ateua viongozi wawili

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi wawili akiwemo, Profesa Eleuther Alphonce Mwageni kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Prof. Mwageni ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Ardhi (ARU) na anachukua nafasi ya Prof. Esther Ishengoma ambaye amemaliza muda wake.

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema, uteuzi wa Profesa Mwangeni umeanza jana Jumatatu, tarehe 07 Juni, 2021.

Msigwa amesema, Rais Samia amemteua Dk. Neema Bhoke Mwita kuwa Mjumbe wa Baraza la Ushindani (FCC).

Dk. Mwita amechukua nafasi ya Dk. Theodora Nemboyao Mwenegoha ambaye ameteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Uteuzi wa Dk. Mwita umeanza leo Jumanne.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!