Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua viongozi wanne
Habari za Siasa

Rais Samia ateua viongozi wanne

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wanne. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Uteuzi huo, ameufanya leo Jumanne tarehe 30 Machi 2021, ukiwa ni uteuzi wa kwanza tangu alipoingia madarakani 19 Machi 2021, baada ya aliyekuwa Rais John Pombe Magufuli kufariki dunia 17 Machi 2021.

Baada ya kifo hicho, Samia aliyekuwa makamu wa Rais, aliapishwa kuwa Rais wa Tanzania.

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imeeleza, uteuzi wa viongozi hao, umeanza jana Jumatatu tarehe 29 Machi 2021.

Walioteuliwa ni; Dk. Florencs Turuka kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma.

Dk. Turuka anachukua nafasi ya Dk. Charles Msonde ambaye amemaliza muda wake.

Pili, Rais Samia amemteua Mhandisi Richard Masika kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Taasisi ya Uhandisi na Usanifu Mitambo Tanzania (Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organization – TEMDO).

Dk. Masika anachukua nafasi ya Profesa Patrick Makungu ambaye muda wake umekwisha.

Tatu, Rais Samia amemteua Dk. Blandina Robert Lugendo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (Fisheries Education and Training Agency – FETA).

Nne, Rais Samia amemteua Paulina Mbena Nkwama kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (Teacher’s Service Commission).

Kabla ya uteuzi huo, Nkwama alikuwa Katibu Tawala Msaidizi (Elimu) Mkoa wa Kilimanjaro na anachukua nafasi ya Winfrida Rutaindurwa ambaye amemaliza muda wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!