RAIS Samia Suluhu Hassan leo Ijumaa
amemteua Mussa Mohamed Makame, Mkurugenzi Mtendaji, Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri
na Uwekezaji wa Mfuko wa Mafuta na Gesi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Pia Rais Samia amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi hiyo, Dkt. Suleiman Magema Missango – Meneja Msaidizi Kurugenzi ya Utafiti na Sera, Benki Kuu ya Tanzania (BoT); Safiel Fahamuel Msovu – Afisa Fedha Mwandamizi, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC);
Wengine ni Shogholo Charles Msangi – Mkurugenzi wa Kampuni ya Express Microfinance Company Ltd; na Mwanaidi Athuman Mtanda- alikuwa Mhasibu Mkuu wa Serikali.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu , Zuhura Yunus, uteuzi huo umeanza tarelhe 11 Mei 2023.
Leave a comment