Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ateua Ma- DC 2
Habari za Siasa

Rais Samia ateua Ma- DC 2

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya (DC) wawili. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Uteuzi huo, umetangazwa jana Jumanne, tarehe 22 Juni 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Walioteuliwa ni; Suleiman Yusuph Mwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Mwenda anachukua nafasi ya Kenan Kihongosi ambaye kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imemteua kuwa Katibu Mkuu wa umoja wa vijana wa chama hicho (UVCCM).

Kabla ya uteuzi huo, Mwenda alikuwa Katibu Msaidizi Idara ya Oganaizesheni ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu jijini Dodoma.

Aidha, Rais Samia amemteua, Lupakisyo Andrea Kapange kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

Kapange anachukua nafasi ya Dk. Charles Mhina ambaye atapangiwa majukumu mengine.

Kabla ya uteuzi huo, Kapange alikuwa Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Tanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!