RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Said Ally Mohamed kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus.
Kwa mujibu wa taarifa ya Yunus, uteuzi wa Dk. Mohamed aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma za Ufundishaji, Mafunzo na Mitihani katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), umeanza tarehe 23 Februari mwaka huu.
“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Mohamed kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania. Uteuzi huu umeanza tarehe 23 Februari 2023,” imesema taarifa ya Yunus.
Dk. Mohamed anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Charles Msonde ambaye Mei 2022 aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (elimu).
Nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Athuman Amasi tangu kuondoka kwa Dk. Msonde.
Leave a comment