Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Samia ateua Katibu Mtendaji NECTA
Elimu

Rais Samia ateua Katibu Mtendaji NECTA

Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Said Ally Mohamed kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 25 Februari 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus.

Kwa mujibu wa taarifa ya Yunus, uteuzi wa Dk. Mohamed aliyekuwa Mkurugenzi wa Huduma za Ufundishaji, Mafunzo na Mitihani katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), umeanza tarehe 23 Februari mwaka huu.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Mohamed kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania. Uteuzi huu umeanza tarehe 23 Februari 2023,” imesema taarifa ya Yunus.

Dk. Mohamed anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Charles Msonde ambaye Mei 2022 aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI (elimu).

Nafasi hiyo ilikuwa ikikaimiwa na Athuman Amasi tangu kuondoka kwa Dk. Msonde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!