RAIS Samia Suluhu Hassan leo tarehe 20 Januari, 2022 amemteua Suzan William Mkangwa kuwa Kamishna wa Kazi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema uteuzi wake ulianza tarehe 17 Januari, 2022.
Kabla ya uteuzi huo, Suzan alikuwa Mtumishi katika Ofiosi ya Rais Ikulu na anachukua nafasi ya Brigedia Jenerali Francis Ronald Mbindi aliyepangiwa majukumu mengine.
Leave a comment