Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia ateta na muwekezaji mradi wa gesi asilia
Habari Mchanganyiko

Rais Samia ateta na muwekezaji mradi wa gesi asilia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Dutch Shell, Ben Van Beurden, kuhusu masuala ya uwekezaji katika mradi wa gesi asilia iliyosindikwa (LNG). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Samia amefanya mazungumzo hayo leo Jumatatu, tarehe 4 Oktoba 2021, kwa njia ya mtandao, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na Waziri wa Nishati, January Makamba na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor.

Wengine walioshiriki ni, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati Mhandisi Leonard Masanja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dk. James Mataragio.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Jaffar Haniu, Rais Samia amemshukuru  Van Beurden, kwa nia yao njema ya kutaka kuwekeza kwenye mradi huo, ambao utachochea kukuza uchumi wa Tanzania.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Dutch Shell, Ben Van Beurden

“Rais Samia  leo tarehe 04 Oktoba, 2021 amezungumza kwa njia ya mtandao na Ben Van Beurden, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Royal Dutch Shell yenye makao yake makuu nchini Uholanzi,” imesema taarifa ya Haniu.

Kwa upande wake, Van Beurden amesema wanarishishwa na namna Serikali ya Rais Samia, ilivyoboresha mazingira ya uwekezaji katika mradi huo.

“Van Beurden amemshukuru  Rais Samia na kueleza kuwa, wanaridhishwa na jinsi Serikali ya Awamu ya Sita, ilivyoboresha mazungumzo ya uwekezaji kwenye mradi wa Gesi asili iliyosindikwa (LNG) hapa nchini,” imesema taarifa ya Haniu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!