Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia ataka wanawake kuchangamkia fursa vyuo vya ufundi
Habari

Rais Samia ataka wanawake kuchangamkia fursa vyuo vya ufundi

Spread the love

 

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wanawake kujifunza mafunzo ya ufundi wa ushonaji wa nguo kwa kuwa ni mojawapo ya sekta ambayo inaajiri wanawake wengi zaidi ikilinganishwa na wanaume. Anaripoti Mwandishi Wetu .. (endelea).

Pia amevitaka vyuo vya mafunzo stadi na vinavyotoa mafunzo ya fushonaji vifundishe viongozi jitihada ili kuzalisha watu wenye sifa ya kuajiriwa.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leotarehe 11 Januari, 2022 – Chumbuni Visiwani Zanzibar wakati akizindua kiwanda cha nguo cha Basra Textile Mills, ikiwa ni sehemu ya maonyesho ya kuelekea miaka 58 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Amesema uzoefu unaonyesha nchi nyingi za Bara la Asia watenda kazi wengi wanaoajiriwa kwenye viwanda vya nguo ni wanawake.

“Hii ni kwasababu wanawake ni watulivu na waangalifu sana. Kwasababu unaposhona nguo ya kimataifa haitaki papara, inataka utulie ufikie vigezo vinavyohitajika na pia mikono yao ni laini kuweka vifungo, kutunga sindano na vitu vingine.

“Lakini fikirieni mikono ya mwanaume ishike vifungo! Kwahiyo hapa ni fursa ya ajira kwa wanawake wengi. Kinamama kasomeni mshone fursa iko hapa,” amesema Rais Samia.

Aidha, amesema matarajio ni kwamba siku za usoni kuacha kuagiza bidhaa hizo kutoka nje hasa nguo za watoto pamoja na kusafirisha kwenda soko la ukanda wa Afrika Mashariki na baadae eneo la ukanda wa SADC.

“Kwahiyo hii ni fursa nzuri kwetu kutumia masoko mawili kupeleka bidhaa zetu huko. Muione fursa hii ili katika kipindi hiki ambapo muwekezaji anajiandaa kuwekeza phase ya pili tuwe tumeshajiandaa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!