Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ataka PF3 iondolewe kunusuru maisha ya watu
Habari za Siasa

Rais Samia ataka PF3 iondolewe kunusuru maisha ya watu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, ameshauri kifungu cha Sheria ya Jeshi la Polisi  kinachokataza majeruhi wa ajali kutibiwa hadi wapate Fomu ya Polisi ya Matibabu (PF3), kiondolewe ili kuokoa maisha ya watu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kiongozi huyo wa Tanzania ametoa wito huo leo Jumanne tarehe 18 Mei 2021, akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa Chuo cha Ushonaji cha Polisi Kurasini mkoani Dar es Salaam.

Rais Samia amesema watu wengi hupoteza maisha kutokana na kuchelewa kupata matibabu kufuatia kukosa fomu hiyo.

IGP Simon Sirro

“Suala la wanaopata ajali, wanaumia kwa viwango tofauti mwingine anaumia anapofika hospitali ahudumiwe haraka.  Lakini kwa sheria yetu hawezi kuhudumiwa mpaka iende  PF3, watu wanafia pale hospitalini,”  amesema Rais Samia na kuongeza:

“Mtu anapopata ajali wa naomuokota na kupaniki mbio hospitali, hawakumbuki kurudi polisi. Naomba hii sheria muiangalie kwamba mtu anapofikishwa hospitali apate huduma mambo mengine ya kipolisi yaendelee, tunapoteza watu kwa sababu ya kipengele kidogo cha PF3.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!