Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia ataka mfuko wa pembejeo kukabili mfumuko wa bei
Habari Mchanganyiko

Rais Samia ataka mfuko wa pembejeo kukabili mfumuko wa bei

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wizara ya Kilimo ianzishe mfuko wa pembejeo na wa maendeleo ya kilimo, kwa ajili ya kukabiliana na changamoto ya mfumuko wa bei za pembejeo kwa wakulima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Rais Samia ametoa agizo hilo leo Jumatatu, tarehe 4 Aprili 2022, akizindua ugawaji vitendea kazi kwa maafisa ugani kilimo, jijini Dodoma.

“Nitoe agizo muanzishe mifuko ya mzunguko, ambao mnaona utakuwa wa pembejeo na wa pili wa maendeleo ya kilimo. Madhumuni tunapoenda kupata shida ya pembejeo zinapopanda bei, mfuko ushushe presha ya bei kwa wakulima. Wakulima wetu wasiende kupata kadhia ya kulipa pesa nyingi kupata pembejeo,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema atazungumza na uongozi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ili kuangalia namba ya kupata fedha za kuendesha mifuko hiyo.

Pia ameagiza jumuiya za watu wanaofanya kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia mabwawa ya Serikali, waanze kutozwa fedha kwa ajili ya kutunisha mifuko hiyo.

Rais Samia ameiagiza Wizara ya Kilimo, ifumue muundo wa Tume ya Umwagiliaji, ili kuanzisha ofisi za umwagiliaji ngazi ya wilaya kwa ajili ya kufikisha huduma karibu na wananchi.

Rais Samia ametoa maagizo hayo baada ya Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, kumuomba atoe fedha kiasi cha Sh. 150 bilioni, kwa ajili ya kutoa ruzuku za pembejeo kwa wakulima, katika kipindi hiki ambacho kuna mfumuko wa bei ya bidhaa hiyo.

Katika hatua nyingine, Rais Samia amewaomba wabunge waibebe sekta ya kilimo bungeni, ikiwemo kwa kupitisha bajeti ya Wizara ya Kilimo.

“Wabunge mko hapa, mmesikia mipango ya wizara, Serikali imeongeza bajeti… nawaombeni sana tubebeni sekta ya kilimo, sekta nyingine zinakwenda vizuri. Kwenye kilimo pitisheni kwa kauli moja tuweze kutekeleza,” amesema Rais Samia.

Pia, Rais Samia ameagiza eneo litakalobaki kwenye ujenzi wa Bwawa la Ufuaji Umeme la Mwalimu Julius Nyerere, kwenye Mto Rufiji, litumike kwa ajili ya shughuli za kilimo.

“Wizara ya Fedha na Wizara ya Ardhi, mligawe litakwenda kwa ajili ya mazao.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!