Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia ataja sababu panga pangua viongozi wa Serikali
Habari za Siasa

Rais Samia ataja sababu panga pangua viongozi wa Serikali

Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania
Spread the love

 

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amesema kutoelewana miongoni mwa viongozi wa Serikali na wasaidizi wao ndiyo sababu kubwa ya kupangua safu ya uongozi katika wizara mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amebainisha hayo leo Jumatatu tarehe 27 Februari 2023 mara baada ya kuwaapisha viongozi wapya aliowateua jana wakiwemo Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makati Wakuu wa wizara mbalimbali.

Mkuu huyo wa nchi amesema atahakikisha panga pangua hiyo itakuwa ni ya mwisho inayotokana na kutoelewana kwa watendaji wao wakuu wa serikali.

Amesema endapo ikitokea tena kutoelewana kwa viongozi basi wote hawana budi kuondoshwa badala ya kupanguliwa na kwamba watateuliwa wengine wapya.

“Likijitikeza tena inamaana hamuwezani hamuwezi kufanya kazi kwahiyo wote mtakwenda kama ni Katibu Mkuna Naibu wake mtakwenda wote, Waziri na Naibu wake mtakwenda wote…nataka nikiwapanga mfanye kazi kwasababu sioni sababu ya kutokuelewana,” amesema Rais Samia

Amesema viongozi hao watapewa semina elekezi itakayofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 1 Machi 2023 ambapo watapewa maelekezo yakutosha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!