RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amesema kutoelewana miongoni mwa viongozi wa Serikali na wasaidizi wao ndiyo sababu kubwa ya kupangua safu ya uongozi katika wizara mbalimbali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Amebainisha hayo leo Jumatatu tarehe 27 Februari 2023 mara baada ya kuwaapisha viongozi wapya aliowateua jana wakiwemo Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makati Wakuu wa wizara mbalimbali.
Mkuu huyo wa nchi amesema atahakikisha panga pangua hiyo itakuwa ni ya mwisho inayotokana na kutoelewana kwa watendaji wao wakuu wa serikali.
Amesema endapo ikitokea tena kutoelewana kwa viongozi basi wote hawana budi kuondoshwa badala ya kupanguliwa na kwamba watateuliwa wengine wapya.
“Likijitikeza tena inamaana hamuwezani hamuwezi kufanya kazi kwahiyo wote mtakwenda kama ni Katibu Mkuna Naibu wake mtakwenda wote, Waziri na Naibu wake mtakwenda wote…nataka nikiwapanga mfanye kazi kwasababu sioni sababu ya kutokuelewana,” amesema Rais Samia
Amesema viongozi hao watapewa semina elekezi itakayofanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 1 Machi 2023 ambapo watapewa maelekezo yakutosha.
Leave a comment