Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia arejea Tanzania
Habari za Siasa

Rais Samia arejea Tanzania

Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania amemaliza ziara yake ya siku tatu nchini Misri na kurejea nchini mwake leo Ijumaa, tarehe 12 Novemba 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam …(endelea).

Rais Samia aliyeondoka Jumatano ya tarehe 10 Novemba 2021 kwenda Cairo, Misri kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Abdel Fattah Al Sisi.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amepokelewa na viongozi mbalimbali akiwamo makamu wake, Dk. Philip Mpango.

Akiwa Misri, pamoja na mambo mengine alifanya mazungumzo na mwenyeji wake katika maeneo kadhaa ya ushirikiano kati ya Tanzania na Misri ikiwemo Nyanja za diplomasia, uchumi, siasa, elimu, utalii na huduma za kijamii.

Pia, Rais Samia na mwenyeji wake, walishuhudia utiaji saini wa mkataba mmoja na hati saba za makubaliano kati ya Tanzania na Misri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!