Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia apokea tuzo ya Babacar Ndiaye, amtaja Magufuli
Habari za Siasa

Rais Samia apokea tuzo ya Babacar Ndiaye, amtaja Magufuli

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema tuzo ya Babacar Ndiaye ya 2022, inayotolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa ajili ya kutambua nchi iliyofanya vizuri katika ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji, alipaswa kupewa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkuu huyo wa Tanzania, ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 25 Mei 2022, jijini Accra nchini Ghana, baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo kwa niaba ya Serikali yake ya Awamu ya Sita.

“Nikitambua napokea tuzo hii nikiwa bado siamini kwamba tuzo hii inaweza kuwa ya mtu binafsi, mimi naamini tuzo hii inatakiwa iwe ya mtu mmoja lakini anayestahili kuliko wote Tanzania ni Dk. John Magufuli,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema, jitihada za ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji zilianzishwa katika awamu tano za uongozi zilizopita, lakini katika jitihada hizo Hayati Magufuli ajitokeza zaidi kwa kuwa alikuwa Waziri wa Ujenzi katika Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Hayati Benjamin Mkapa na Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Jakaya Kikwete.

Akizungumzia maendeleo ya Bara la Afrika, Rais Samia amewashauri wakuu wa nchi kuweka mikakati madhubuti ya usimamizi wa rasilimali za bara hilo ikiwa pamoja na kuimarisha ukanda wa biashara, ili zinufaishe wananchi.

Ili kufanikisha hilo, Rais Samia ameshauri nchi za Afrika kuimarisha miundombinu ya usafirishaji hasa barabara na reli, kwani ni kigezo muhimu katika kuunganisha bara hilo na fursa za kiuchumi.

1 Comment

  • Duh!
    Mama umesema kweli.
    Je, utaikabidhi kwa familia ya Hayati Magufuli iwekwe kwenye makumbusho yake?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!