RAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la Mawaziri, Kwa kuwahamisha mawaziri wawili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Leo tarehe 1 Aprili 2023 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Zuhura Yunus, Rais Samia amemhamisha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na utawala Bora, kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu).
Taarifa hiyo inasema kuwa , Mhagama anachukua nafasi ya George Simbachawene, ambaye Rais Samia amemteua kwenda katika wizara aliyotoka ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Nchi, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
“Uteuzi Huu umeanza tarehe 1 Aprili 2023 na mawaziri wateule wataapishwa tarehe 2 Aprili 2023, saa 3 asubuhi, Ikulu jijini Dar es Salaam,” imesema taarifa ya Yunus.
Na wale aliowaita STUPID bado wanakula bata?