Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amwapisha Mdolwa kuwa Balozi
Habari za Siasa

Rais Samia amwapisha Mdolwa kuwa Balozi

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Yusuf Tindi Mndolwa kuwa Balozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mdolwa, ameapishwa leo Jumatatu, tarehe 19 Aprili 2021, Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali, akiwemo Makamu wa Rais, Dk. Philip Mpango.

Mdolwa aliteuliwa juzi Jumamosi kuwa Balozi na akamteua pia kuwa Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol) katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Pia, Rais Samia alimteua Benedict Ndomba kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).

Kabla ya uteuzi huo, Ndomba alikuwa Mkurugenzi wa Miundombinu na Operesheni wa eGA na anachukua nafasi ya Dk. Jabir Bakari Kuwe ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Wateuliwa hao, wamekula kiapo cha uaminifu kwa viongozi wa umma, kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili, Jaji Sivangilwa Mwangesi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!