Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amwalika Rais wa Marekani
Habari za SiasaKimataifa

Rais Samia amwalika Rais wa Marekani

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemwalika Rais wa Marekani, Joseph Biden kutembelea nchini humo ili kuzidi kuimarisha uhusino uliopo kati ya nchi hizo mbili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Ametoa mwaliko huo, jana Jumanne, tarehe 06 Julai, 2021, alipofanya mazungumzo kwa simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken.

Blinken amempongeza, Rais Samia kwa kushika hatamu ya uongozi nchini na kumhakikishia kuwa Serikali ya Marekani itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuleta maendeleo kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) kwa kuzingatia vipaumbele vya nchi.

Joe Biden, Rais wa Marekani

Katika mazungumzo hayo, Blinken amepongeza Rais Samia kwa hatua anazozichukua kukabiliana na ugonjwa wa Corona nchini Tanzania na Marekani ipo tayari kuisaidia Tanzania katika kukabiliana na ugonjwa huo.

Aidha, Blinken amepongeza jitihada za Rais Samia katika kuimarisha Demokrasia nchini ikiwa ni pamoja na azma yake ya kukutana na kushirikiana na vyama vya siasa pamoja na kusimamia Uhuru wa vyombo vya habari.

Pia, amepongeza uboreshaji wa mazingira ya ufanyaji biashara na kuahidi kuwa hali hiyo imeivutia Marekani kushawishi wawekazaji wake kuja kuwekeza nchini.

Kwa upande wake, Rais Samia ameshukuru kwa pongezi na kuahidi kuwa Serikali yake itaendelea kushirikiana na Serikali ya Marekani kukuza uhusiano baina ya nchi hizi mbili katika majukwaa mbalimbali ya kimataifa.

1 Comment

  • Rais wetu kuzungumza na waziri wa mambo ya nje wa Marekani? Protokali ya wapi? Kwanini Biden asizungumze na Mama? Tusijidhalilishe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!