Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amvua ubalozi Dk. Slaa
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia amvua ubalozi Dk. Slaa

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan leo Ijumaa amemvua hadhi ya Ubalozi Dk. Wilbroad Slaa kuanzia tarehe 01 Septemba, 2023.

Dk. Slaa aliteuliwa kuwa Balozi tarehe 23 Novemba 2017 na Rais awamu ya Tano hayati, Dk. John Magufuli. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa  iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imethibitisha madai ya Dk. Slaa kuwa tangu aanze kupinga mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi kati ta Serikali ya Tanzania na Dubai, amekuwa akipokea vitisho vya kuvuliwa hadhi ya ubalozi.


Dk. Slaa ambaye amekuwa kinara wa kupinga mkataba huo ambao pia Dubai kupitia kampuni ya DP World itawekeza kwenye bandari za Tanzania, tayari alikamatwa pamoja na wenzie kutokana na tuhuma mbalimbali za uhaini kisha kuachiwa kwa dhamana.

Tarehe 12 Julai mwaka huu, Mbunge huyo wa zamani wa Karatu na Katibu mkuu mstaafu wa Chadema, alisema baada ya kupiga kelele kuhusu mkataba huo amepigiwa simu na kutishiwa na watu kutoka serikalini kwamba akae kimya na akiendelea kupiga kelele watamvua hadhi ya ubalozi mara moja!

“Najua maneno hayo ni makali… nimepokea vitisho na mimi pia sio kwa mawakili tu, wengine wakasema ubalozi wako tutachukua, nawaambia chukueni sasa hivi…siishi kwa ajili ya ubalozi. Nimesema sina chama najiamini najau ninachosimamia.

“Nitasema siku zote, CCM au Chadema ikifanya mema nitapongeza, anayeharibu yeyote nitamsema bila kumung’unya maneno, bila kuona aibu na kwa hili hakuna aibu tutakwenda wote,” alisema Dk. Slaa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!