Rais Samia leo tarehe 10 Januari, 2022 amemuapisha Jaji Jacob Mwambegele kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Anaripoti Mwandishi Wetu (endelea).
Jaji Mwambegele amechukua nafasi ya Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Semistocles Kaijage ambaye amemaliza muda wake.
Jaji Mwambegele aliteuliwa tarehe 23 Disemba mwaka jana ameapishwa Ikulu jijini Dodoma pamoja na viongozi wa taasisi nyingine sambamba na mawaziri walioteuliwa hivi karibuni.
Leave a comment