Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Rais Samia amtumbua kigogo TPA
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia amtumbua kigogo TPA

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko, ili kupisha uchunguzi wa ubadhirifu wa fedha Sh. 3.9 Bilioni, uliofanyika katika mamlaka hiyo.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kiongozi huyo mpya wa Tanzania amechukua hatua hiyo leo Jumapili tarehe 28 Machi 2021, baada ya kupokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020.

CAG Kichere ameikabidhi ripoti hiyo kwa Rais Samia, Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

“Imani yangu ni kwamba, kama kuna ubadhirifu ndani ya shirika na kwa ripoti ile uliyonipa jioni, kuna uibadhirifu Sh. 3.9 Bil. karibu Sh. 4 Bil.
Waziri Mkuu(Kassim Majaliwa) alivyofanya ukaguzi walisimamishwa wa chini, naomba nitoe agizo la kumsimamisha mkurugenzi mkuu wa bandari halafu uchunguzi uendelee,” ameagiza Rais Samia.

Rais Samia amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), Brigedia Jenerali, John Mbungo, kufanya uchunguzi dhidi ya tuhuma hizo.

“Katika ripoti yako nimeona pia ubadhirifu mkubwa umefanywa katika shirika la bandari TAKUKURU hii ni kazi maalumu jishughulishe pale,” ameagiza Rais Samia.

Awali CAG kichere alisema katika ukaguzi wake, amebaini ubadhirifu TPA, na kueleza kwamba, ofisi yake inaendelea na ukaguzi wa ubadhirifu huo.

“Ukaguzi tuliofanya katika mashirika mbalimbali ya Serikali, tumegundua changamoto kadhaa ambazo zinahitaji serikali kukagua, ikiwemo matatizo katika Shirika la Bandari, ubadhirifu ambao tunaendelea kufanya ukaguzi katika maeneo hayo,” amesema CAG Kichere

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!