Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amteua bosi wa zamani SADC kuwa mbunge
Habari za Siasa

Rais Samia amteua bosi wa zamani SADC kuwa mbunge

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua Dk. Stergomena Tax, kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya Jaffari Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu aliyoitoa leo Ijumaa, tarehe 10 Septemba 2021, imesema Dk. Tax ataapishwa kwa mujibu wa sharia na taratibu za Bunge.

Rais Samia amemteua, Dk. Tax takribani wiki mbili zimepita tangu alipomaliza muda wake wa miaka nane ya kuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan

Uteuzi huo kwa Dk. Tax ni wa pili kufanywa kwake na Rais Samia kwani tarehe 13 Mei 2021, aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Uongozi.

Dk. Tax ambaye ni raia wa Tanzania, alianza kutumikia jumuiya hiyo mwaka Septemba 2013, baada ya kuteuliwa katika mkutano wa 33 wa SADC uliofanyika, Lilongwe nchini Malawi.

Dk. Tax, amewahi kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki ya Tanzania kati ya Novemba 2008 hadi August 2013, ikiwa ni katika utawala wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!