Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia amsifu Dk. Magufuli, amtaja Dk. Kikwete, Karume
Habari za Siasa

Rais Samia amsifu Dk. Magufuli, amtaja Dk. Kikwete, Karume

Spread the love

 

RAIS WA Tanzania, Samia Suluhu Hassa, amesifu uongozi wa kutukuka wa mtangulizi wake, Hayati John Magufuli huku akimtaja Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Amani karume kwamba ndiye aliyemuibua. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Akihutubia Bunge leo tarehe 22 Aprili 2021, Rais Samia amesema, mtangulizi wake (Dk. Magufuli), alikuwa kiongozi bora, jasiri na aliyetumikia Taifa lake kwa dhati.

“Dk. Magufuli alikuwa kiongozi hodari, jasiri, shupavu na mwenye maoni ambaye aliipenda nchi yetu na kuitumikia kwa uadilifu mkubwa,” amesema.

Amesema, anashukuru chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kumwamini na kwamba, kutokana na chama hicho, amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amemtaja Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Aman Karume kwamba ndiye aliyemuibua na kumpa nafasi ndani ya serikali yake. Na kwamba, baada ya hapo, Dk. Jakaya Kikwete ambaye ni Rais Mstaafu wa Tanzania alimteua uwaziri pia Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba.

“Nimshukuru Rais Kikwete ambaye alinipa malezi haya, namshukuru kwa kunipa uwaziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano na kuniamini katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba.

“Namshukuru Dk. Magufuli kwa kuniamini na kuwa mgombea mwenza wake kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na 2020, kuniamini kwake kumeniwezesha kuwa mwanamke wa kwanza nchini kushika wadhifa wa kamamu wa rais na sasa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!