Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia ampongeza mshindi wa Nobel aliyejinyakulia bilioni 2
Habari Mchanganyiko

Rais Samia ampongeza mshindi wa Nobel aliyejinyakulia bilioni 2

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

SAMIA Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania, amempongeza, Abdulrazak Gurnah kwa kutwaa tuzo ya amani ya Nobel katika fasihi 2021, kutokana na kuangazia suala la ukoloni na athari zake katika utunzi wake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Gurnah (73) ambaye ni Mwandisi wa riwaya nchini Tanzania alitangazwa mshindi jana Alhamisi, tarehe 7 Oktoba 2021 na Kituo hicho kinachotoa tuzo hizo za Nobel.

Profesa huyo wa fasihi ametwaa tuzo hiyo iliyotolewa na kituo hicho cha Sweden ina thamani ya corona milioni 10 za taifa hilo sawa na Sh bilioni 2.6.

Mara baada ya kutangazwa mshindi, Rais wa Tanzania, Samia ametumia ukurasa wake wa twitter kumpongeza mwana fasihi huyo.

“Nakupongeza Bw. Abdulrazak Gurnah kwa kutunukiwa Tuzo ya Nobel katika fasihi ya mwaka 2021. Tuzo hii ni heshima kwako, Taifa letu la Tanzania na Afrika,” ameandika Rais Samia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!