Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia kaka yake Mbowe
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia amlilia kaka yake Mbowe

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kwa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania nchini humo-Chadema kufuatia kifo cha kaka yake, Charles Mbowe. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Charles amefikwa na mauti usiku wa kumakia leo Jumatano, tarehe 8 Julai 2021, katika Hospitali ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro.

Rais Samia ametumia ukurasa wake wa Twitter kutuma salamu za rambirambi akisema “Nakupa pole Ndg. Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA) na wafiwa wote kwa kuondokewa na ndugu yenu mpendwa Charles Mbowe.”

“Nawaombea moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki cha majonzi. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina,” amesema Rais Samia

Mapema leo Alhamisi mchana, Freeman amesema, kaka yake atazikwa nyumabani kwao Machame, Jumatatu tarehe 12 Julai 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!