Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia kaka yake Mbowe
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia amlilia kaka yake Mbowe

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za rambirambi kwa Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania nchini humo-Chadema kufuatia kifo cha kaka yake, Charles Mbowe. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Charles amefikwa na mauti usiku wa kumakia leo Jumatano, tarehe 8 Julai 2021, katika Hospitali ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro.

Rais Samia ametumia ukurasa wake wa Twitter kutuma salamu za rambirambi akisema “Nakupa pole Ndg. Freeman Mbowe (Mwenyekiti wa CHADEMA) na wafiwa wote kwa kuondokewa na ndugu yenu mpendwa Charles Mbowe.”

“Nawaombea moyo wa subira, uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki cha majonzi. Bwana ametoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, Amina,” amesema Rais Samia

Mapema leo Alhamisi mchana, Freeman amesema, kaka yake atazikwa nyumabani kwao Machame, Jumatatu tarehe 12 Julai 2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!