Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia amlilia Askofu Mwenisongole, kuzikwa Desemba 30
Habari Mchanganyiko

Rais Samia amlilia Askofu Mwenisongole, kuzikwa Desemba 30

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametoa salamu za pole kufutia kifo cha Askofu Mkuu mstaafu wa Tanzania Assemblies of God (TAG), Mchungaji Ranwell Mwenisongole. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Askofu Mwenisongole aliyekuwa Mchungaji Kiongozi wa TAG Upanga Jijini Dar es Salaam, alifikwa na mauti jana Jumamosi, tarehe 25 Desemba 2021.

Leo Jumapili, Rais Samia ametumia ukurasa wake wa Twitter kuzungumzia kifo hicho akasema,”nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Askofu Dkt. Ranwell Mwenisongole aliyekuwa Askofu Mkuu wa Awamu ya Pili TAG.”

 

“Pole kwa familia, Askofu Mkuu Dkt. Barnabas Mtokambali, wana TAG wote, ndugu, jamaa na marafiki. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.”

Askofu mwenisongole alikuwa akisumbuliwa na kisukari na shikikizo la damu na msiba upo nyumbani kwake, Mbezi-Mkonde jijini Dar es Salaam.

Mwili wake utaagwa tarehe 29 Desemba 2021, Kanisa la TAG Upanga kuanzia saa 3 asubuhi kisha utasafirishwa kwa maziko yatakayofanyika 30 Desemba 2021, Jimbo la TAG Songwe, Wilaya ya Vwawa mkoani Songwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!